Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa vyuo vikuu vyenye taaluma ya sayansi na tiba vinakuwa na hospitali za kufundishia?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri nikupongeze yaani kwa hilo kwa leo nikupongeze, lakini nina swali moja tu la nyongeza. Chuo cha Dodoma ambacho ni kikubwa Afrika Mashariki, na ni kikubwa kweli, kina pia hizo kozi; na kwa hiyo katika kuendelea kufata hizi Sera za Kimataifa, je, Serikali ni lini itaanza kujenga sasa maana yake mmesema vyuo vingine vitajengwa lakini kwa Chuo hiki cha UDOM ni lini chuo hicho mtaanza kujenga teaching hospital?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKINOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru kwa pongezi alizotoa Mheshimiwa Mbunge na pongezi hizi moja kwa moja ziende kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye ndiye ambaye amewezesha mambo haya yote kuweza kutokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya msingi, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma wale ambao wanasoma fani au kozi hizi za tiba, wanafanya mafunzo yao kwa vitendo katika hospitali yetu ya Benjamin Mkapa, ambayo iko karibu kabisa na Chuo hiki cha Dodoma. Lakini vilevile wanafanya mafunzo yao katika Hospitali yetu ya Milembe hapa Dodoma. Pia wanafanya mafunzo yao kwa vitendo kwenye hospitali za mikoa ya Dodoma, Singida Pamoja na Iringa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, na nilithibitishie hapa kwamba Serikali inaendelea na jitihada za kuona vyuo hivi vinakuwa na hospitali zake zenyewe za kufundishia ikiwemo na chuo hiki cha Dodoma. Kwa hiyo tutaendelea kutafuta fedha ili takwa hili la kimafunzo liweze kufikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.