Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Water and Irrigation Wizara ya Maji 278 2023-05-09

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati miundombinu chakavu ya maji na kuhakikisha upatikanaji wa maji ya kutosha katika Mji wa Mbinga?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza ukarabati wa miundombinu chakavu katika Mji wa Mbinga. Kazi zinazoendelea ni pamoja na ukarabati wa mabomba ya maji umbali wa kilometa 21, ukarabati wa kitekeo cha maji Ndengu na ununuzi wa dira za maji 2,500 kwa ajili ya kuunganisha wateja wapya. Utekelezaji wa kazi hizo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuhakikisha wakazi wa Mji wa Mbinga wanapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza, Serikali imekamilisha usanifu wa Mradi wa Maji Mbinga utakaohusisha ujenzi wa vitekeo viwili vya maji, matenki matatu yenye jumla ya ujazo wa lita 450,000 na ulazaji wa mabomba umbali wa Kilometa 83. Utekelezaji wa mradi huo utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.