Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 21 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 279 2023-05-09

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

Je, lini hatua iliyobakia katika mchakato wa kupata Katiba Mpya itakamilishwa?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu sasa swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua umuhimu wa mchakato wa kupata katiba mpya aliunda kikosi kazi kilichoongozwa na Profesa Mukandara ambacho pamoja na masuala mengine, ilikuwa ni kuhuisha mchakato wa Katiba mpya. Katika hilo, kikosi kazi hicho kimetoa mapendekezo ya hatua sita za kufuatwa katika kukamilisha mchakato wa kupata Katiba Mpya. Hatua hizo ni hizi zifuatazo: -

(i) Kuwepo kwa mjadala wa Kitaifa wa kupata muafaka wa masuala ya msingi;

(ii) Kuhuisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba;

(iii) Kuundwa kwa Jopo la Wataalam wa kuandaa Rasimu ya Katiba;

(iv) Rasimu ya Katiba kupitishwa na Bunge;

(v) Kutoa elimu ya uraia; na

(vi) Rasimu ya Katiba kupigiwa kura na wananchi.

Mheshimiwa Spika, baada mapendekezo ya kikosi kazi, tarehe 6 Mei, 2023, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alimuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa kuitisha Kikao Maalum cha Baraza la Vyama vya Siasa wakiwemo wadau mbalimbali kujadili mapendekezo ya kikosi kazi na kupendekeza taratibu za kuzingatia katika kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya. Ahsante.