Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, lini hatua iliyobakia katika mchakato wa kupata Katiba Mpya itakamilishwa?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. pamoja na majibu ya Serikali, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwenye mapendekezo ambayo ameyataja hapo sikuona suala zima la elimu kwa raia, kwa wananchi, kwa maana Katiba si mali ya wanasiasa pekee ni mali ya wananchi. Je, Serikali imejipangaje kuanzisha elimu japo kwa Katiba hii iliyopo ya mwaka 1977 ambayo wananchi wengi hawaifahamu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; wakati wa rasimu ya Mheshimiwa Warioba, mwaka 2012, mpaka sasa ni takribani miaka kumi na moja, wapo Watanzania ambao wakati ule walikuwa na umri mdogo na sasa wametimiza miaka 18.

Je, Serikali katika mapendekezo hayo itazingatia kwenda upya kutafuta maoni ya wananchi ili kujenga wigo mkubwa wa ukusanyaji wa maoni?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza kuhusu elimu kwamba, itolewe ya Katiba iliyopo. Serikali tumejipanga na ndio maana katika bajeti yetu ambayo tuliileta kwenu Waheshimiwa Wabunge tumeweka pia bajeti kwa kazi hiyo. Kwa hiyo Serikali tutatoa elimu ya Katiba iliyopo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, lakini pia Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Katiba hizi zote tutapeleka elimu kwa wananchi ili wazifahamu kabla mchakato huu haujaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, amependa kufahamu pia kama wananchi ambao kipindi kile cha rasimu ya Mheshimiwa Warioba hawakushiriki kutoa maoni yao kwa sababu ya umri, kama kipindi hiki watashirikishwa: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wote wa Tanzania watashirikishwa. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuona hili, ndio maana sasa mchakato huu unaanza ili na wale ambao hawakupata nafasi ya kutoa maoni yao basi na wao waweze kutoa maoni yao.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, lini hatua iliyobakia katika mchakato wa kupata Katiba Mpya itakamilishwa?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Suala la Katiba Mpya ni kilio cha muda mrefu sana kwa Watanzania wote, tukiondolewa sisi wanasiasa. Ni lini Serikali italeta Sheria ya Vyama vya Siasa kuhakikisha hii Katiba Mpya tunapokwenda kwenye hilo tamko ambalo Rais ameliridhia, ataenda kulizungumzia na Watanzania wakafahamu, ni lini tunaanza na tutatumia mbinu gani na mipango gani ambayo Serikali imejipanga kuhakikisha Katiba hii inakuwa ya wananchi jumuishi na maoni yanachukuliwa kwa ujumla wake? Tunaomba commitment ya Serikali iseme itaanza lini na itatumia mbinu gani kuhakikisha Katiba hii inaenda kusimama upya tena?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuungana na Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote ambao wamempongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali sasa mapendekezo ya kikosi cha Baraza la Vyama vya Siasa na wadau wengine kuhakikisha tunaanza mchakato wa Katiba Mpya, ikiwa ni pamoja na kuhuisha na kutungwa kwa sheria zinazohusu uchaguzi hapa nchini Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba, kwa kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Rais, tayari Baraza la Vyama vya Siasa linashirikiana na wadau mbalimbali na limeshaweka mpango kazi kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini na ofisi nyingine zinazohusika ili kuhakikisha kabla mwaka huu wa 2023 sheria zote zinazohusu uchaguzi Bunge lako tukufu lipate nafasi ya kuzipitia, kuzitunga na kuzifanyia marekebisho kama itabidi kufanya hivyo. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, Serikali imezingatia sana maoni hayo na tayari tumeshajipanga kwa utekelezaji wa mabadiliko ya sheria hizo. (Makofi)