Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 302 2023-05-12

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itahakikisha Watanzania wanaofanya kazi kwenye Kampuni za Kichina wanalipwa vizuri kwa mujibu wa sheria?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria za Kazi ili kulinda haki za wafanyakazi. Aidha, katika kuendelea kuboresha maslahi ya wafanyakazi wa sekta binafsi, Serikali kupitia Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara cha Sekta Binafsi imefanya utafiti na kuboresha kima cha chini cha mishahara ya sekta binafsi, viwango hivyo vipya vya mishahara vilitangazwa kupitia Gazeti la Serikali Namba 687 la tarehe 25 Novemba, 2022 na utekelezaji wake umeanza rasmi tarehe 01 Januari, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na taasisi nyingine zinazohusika na masuala ya kazi itaendelea kuhakikisha kuwa waajiri wanatekeleza ipasavyo viwango vya mishahara vilivyotangazwa kwa kufanya kaguzi za mara kwa mara katika maeneo ya kazi na kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi ili uelewa wao katika kutekeleza Sheria za Kazi unafanyika. Aidha, ofisi imeendelea kuchukua hatua dhidi ya waajiri wanaobainika kukiuka Sheria za Kazi hususan ulipaji wa mishahara kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria.