Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 304 2023-05-12

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa Fedha za ujenzi wa Vituo vya Afya katika Kata za Mnongodi na Nyundo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitenga Shilingi Bilioni 117 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya kimkakati kwenye Kata 234 nchini. Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ilitengewa kiasi cha Shilingi Milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kitaya. Ujenzi wa Kituo hicho upo hatua za ukamilishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya kwenye Kata za Kimkakati nchini ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Vituo vya Afya kwenye Kata za Mnongodi na Nyundo.