Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa Fedha za ujenzi wa Vituo vya Afya katika Kata za Mnongodi na Nyundo?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili.

Mosi, kwa kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya Kitaya umeshakamilika, je, ni lini Serikali sasa itapeleka vifaatiba na wataalam ili huduma ziweze kutolewa?

Swali langu la pili, katika Bajeti ya TAMISEMI ambayo tumepitisha hivi karibuni zimetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vipya vya afya. Je, Serikali inatoa tamko gani sasa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Nyundo au Mnongodi au Kata za kimkakati katika Jimbo letu la Nanyamba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la kwanza la nyongeza la Mheshimiwa Chikota la Kituo cha Afya Kitaya. Serikali imetenga katika mwaka wa fedha huu 2023/2024 shilingi milioni 400 kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Nanyamba kwa ununuzi wa vifaatiba kwa ajili ya zahanati na vituo vya afya. Sasa ni maamuzi ya kwao wao kwamba shilingi milioni 400 hizi wazi-allocate wapi kwenye zahanati zipi, vituo vya afya vipi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kupata vituo vya afya. Tutaangalia katika bajeti iliyotengewa kwa mwaka wa fedha huu 2023/2024 tuone Nanyamba imetengewa vituo vya afya vingapi lakini kama haijatengewa katika mwaka wa fedha huu Serikali itahakikisha inatenga fedha kwa ajili ya vituo vya afya vya Nanyamba katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.