Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 305 2023-05-12

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi Mkoani Mara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 Mkoa wa Mara ulipata walimu 531 kwa shule za Msingi na Sekondari. Kati yao walimu wa masomo ya sayansi walikuwa 197. Ni dhamira ya Serikali kuendelea kuajiri na kuongeza idadi ya walimu wa sayansi ili kuendana na malengo yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI tayari imetenga nafasi za ajira za walimu na watumishi wa kada ya afya kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo jumla ya nafasi 13,130 ni za kada ya elimu na kipaumbele ni masomo ya sayansi. Waombaji watapangiwa vituo vya kazi kwa kuzingatia maeneo yenye upungufu mkubwa ukiwemo Mkoa wa Mara.