Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi Mkoani Mara?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Naishukuru Serikali kwa kutuletea walimu wa sayansi 197, lakini bado tuna upungufu mkubwa sana wa walimu wa masomo ya sayansi 889; je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mkoa wa Mara ili waweze kutatua changamoto hii iliyowakabili na watoto wao waweze kufaulu vizuri?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa walimu wengi wa masomo ya sayansi ni walimu wa jinsia ya kiume: Je, Serikali haioni haja ya kuwa na program maalum ya kuwawezesha watoto wa kike kufundisha masomo ya sayansi? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Chomete, la kwanza la upungufu mkubwa wa walimu wa sayansi katika Mkoa wa Mara; kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba tunaajiri walimu 13,130 na tutazingatia maeneo yenye upungufu mkubwa hapa nchini ikiwemo Mkoa wa Mara. Hivyo nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba Mkoa wa Mara nao upo katika mikoa ya kipaumbele kupata walimu hawa wa sayansi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali la pili, nitoe rai kwa watoto wa kike waweze kwenda kwenye vyuo hivi vya ualimu na kusomea kufundisha masomo ya sayansi, ili tuweze kupata pool kubwa ya maombi ya watoto wa kike wanaoenda kufundisha masomo ya sayansi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tena kwamba katika ajira hizi mpya, tutahakikisha wale walimu ambao wanakidhi vigezo na ni walimu wa sayansi wanaajiriwa katika mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa tatizo la upungufu wa walimu wa sayansi Mkoani Mara?

Supplementary Question 2

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa tunakubaliana kwamba tuna tatizo kubwa la walimu wa sayansi nchini na pia tunatambua kuna maendeleo ya sayansi na teknolojia: Ni kwa nini Serikali isione namna ambavyo inaweza kutumia TEHAMA kwa ajili ya kuhakikisha kwamba inatatua tatizo la walimu kwa mwalimu mmoja kuweza kufundisha shule nyingi kwa wakati mmoja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa TEHAMA, na ndiyo maana Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ilitoa vishikwambi kwa walimu wote kama kianzio cha kwenda kwenye TEHAMA kwa walimu hawa. Kadiri siku zinavyokwenda, kuna shule ambazo zinajengwa za kimkakati kama shule ya mfano iliyokuwepo hapa Iyumbu Jijini Dodoma ambazo zitakuwa ni shule za TEHAMA kuweza kufundisha wanafunzi wetu wengi zaidi, na miaka inavyokwenda, tutazidi kuongeza kama Serikali.