Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 306 2023-05-12

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuboresha Kituo cha Afya Igurusi ili upasuaji uweze kufanyika katika kituo hicho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya Igurusi kilijengwa mwaka 1966 na kuanza kutoa huduma katika ngazi ya zahanati hadi ilipofika mwaka 2010 kilipopandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya. Aidha, miundombinu ya kituo hiki ni michache na iliyopo ni chakavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, imefanya uchambuzi na kupata vituo vya afya vikongwe 193 nchini kote ambavyo vinahitaji kufanyiwa ukarabati na kuongezewa majengo.

Mheshimiwa Naibu Spika, uhakiki umefanyika kutambua vituo vya afya vikongwe na Serikali iko kwenye mchakato wa kutafuta fedha ili kuvikarabati vituo hivyo.