Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuboresha Kituo cha Afya Igurusi ili upasuaji uweze kufanyika katika kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na uchambuzi mzuri uliofanyika na Serikali, wananchi wa Igurusi wanapata shida hasa wazazi wanapokuwa na uzazi pingamizi: Je, ni lini sasa maboresho yataanza kufanyika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, kuna mpango gani wa kupeleka vifaa tiba katika Kituo cha Afya cha Chimala ili waweze kusaidiwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali lake la kwanza la lini maboresho yatafanyika, kama nilivyoshasema kwenye majibu yangu ya msingi, ni kwamba tumefanya tathmini na kugundua kuna vituo vikongwe hapa nchini 193, na hivi sasa tuko katika mchakato wa kutafuta fedha na kuhakikisha tunavikarabati na kuviongezea majengo vituo hivi vya afya ambavyo ni vikongwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye swali lake la pili tutapeleka fedha kadiri ya upatikanaji wa fedha hizo na tutaangalia katika mwaka wa fedha huu ambao bajeti imepitishwa, kama kuna vituo ambavyo viko allocated Mkoa

wa Mbeya, basi tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuona ni namna gani Mbarali nao wanaweza kupata. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuboresha Kituo cha Afya Igurusi ili upasuaji uweze kufanyika katika kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa ni zaidi ya miezi mitano sasa tokea Serikali imepeleka x-ray machines kwa kwenye Vituo vya Afya vya Muriti, Bwisya na Hospitali ya Wilaya ya Nansio, lakini mpaka sasa vifaa hivi havijaanza kutoa huduma kwa wananchi; nini kauli ya Serikali? Nakushukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, jitihada za Serikali zimekuwa ni kubwa sana kupeleka vifaa tiba maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo Muriti na Bwisya kule Ukerewe. Nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kuagiza timu yetu ambayo inazunguka mikoani kutoa mafunzo kwa wataalam wetu kutumia vifaa hivi vya kisasa, wahakakikishe wanafika Ukerewe mara moja na kutoa mafunzo kwa watumishi hawa wa Muriti na kule Bwisya.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuboresha Kituo cha Afya Igurusi ili upasuaji uweze kufanyika katika kituo hicho?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kituo cha Afya cha Endasaki miundombinu yake ni chakavu sana; je, ni lini Serikali itatoa fedha zote zinazohitajika ili kukarabati miundombinu ya kituo hicho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Endasaki pale ambapo upatikanaji wa fedha hizo utakuwepo. Tutaangalia katika mwaka wa fedha huu 2023/2024 kama kituo hiki kimetengewa, ili fedha hizo ziweze kwenda mara moja. Kama hakijatengwa katika mwaka huu wa 2023/2024, tutahakikisha mwaka 2024/2025 kituo hichi kinatengewa fedha.