Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 307 2023-05-12

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga upya na kufanyia ukarabati nyumba zilizo katika Makambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na kuboresha miundombinu mbalimbali kwenye vikosi vya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, ikiwemo ukarabati wa makambi na nyumba za makazi kwa Maafisa na Askari. Ukarabati wa makambi ulianza kutekelezwa tangu mwaka 2020, na unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha na vipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, awamu ya kwanza ya ukarabati inahusu nyumba zilizonunuliwa kimakundi nje ya makambi ya Jeshi, ikiwemo magorofa ya Mwenge, Keko, Nyumba za makazi za Masaki, Kitangili, Nyegezi, Nyamanolo, Tabora, Tanga, Shinyanga na Mtwara. Aidha, ukarabati huu umeanza kutekelezwa katika magorofa ya Mwenge Dar es Salaam na Tanga. Inategemewa ifikapo Desemba, 2023, ukarabati wa awamu hii utakuwa umekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati awamu ya pili utahusisha nyumba zilizopo makambini kwa kuzingatia kanda mbalimbali kwa kuanza na Kanda ya Mashariki, Zanzibar, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Kati, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kusini, Kanda ya Ziwa na kumalizia ukarabati Kanda ya Magharibi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.