Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga upya na kufanyia ukarabati nyumba zilizo katika Makambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa jeshi letu limekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha ulinzi wa nchi na mipaka yake; je, ni maeneo gani kwa Zanzibar ambayo yatapewa kipaumbele katika ujenzi huo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mahanga katika kambi hapa nchini? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Maryam Mwinyi kwa kufuatilia mambo haya ya msingi kwa ustawi wa majeshi yetu. Nimhakikishie, kwenye majibu yangu ya msingi nimeeleza kwamba kwenye ukarabati wa makambi ya awamu ya pili, Zanzibar imo katika vipaumbele. Ninapozungumzia Zanzibar, ni Unguja na Pemba. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwenye awamu ya pili upande wa Zanzibar pia ni kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la pili kuhusu mahanga, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa swali hili. Wizara itafanya tathmini ya mahitaji ya mahanga kote nchini na kuhakikisha katika utekelezaji wa ujenzi wa mahanga pia upande wa Zanzibar wanapewa kipaumbele, ahsante sana.