Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 314 2023-05-12

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka miundombinu katika kivutio cha utalii cha Mount Uluguru Waterfall?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nora Waziri Mzeru, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kujenga miundombinu mbalimbali ikiwemo ngazi kuelekea kwenye Maporomoko ya Hululu, ujenzi wa choo, kuweka miundombinu ya maji, mfumo wa umeme wa jua na mashine ya kusukumia maji na kujenga daraja la mbao kuvuka mto Mgeta. Aidha, Serikali kupitia mradi wa kupunguza athari za UVIKO -19 ilikarabati barabara ya kuelekea kwenye msitu huo wenye urefu wa Kilometa nane kutoka Kijiji cha Kibaoni hadi Bunduki kwenye kivutio cha Maporomoko ya Hululu. Ukarabati huo umewezesha kufikika kwa urahisi kwenye kivutio hicho kwa shughuli za utalii na uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji kuwekeza miundombinu ya utalii katika msitu huo. Miundombinu ya utalii inayoweza kuwekezwa na sekta binafsi ni pamoja na makambi (camp sites), lodge, hotel na maeneo ya burudani, nakushukuru.