Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka miundombinu katika kivutio cha utalii cha Mount Uluguru Waterfall?

Supplementary Question 1

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni lini Serikali itawekeza fedha kwenye kuutangaza Mlima Uluguru kama kivutio kizuri cha utalii?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Kwa kuwa maporomoko haya yanaleta mvutio mkubwa kwa utalii.

Je, ni lini Serikali ina mpango wa kuyatunza na kuhifandhi mazingira yaliyozunguka maporomoko hayo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tutapita vizuri kwenye Jibu la msingi tulisema kwamba Serikali kupitia mfuko wa UVIKO tayari tulishawekeza pale takribani shilingi 214.3 ilikuwa lengo na madhumuni ni kujenga ile miundombinu ya barabara ya kilomita nane kutoka barabara kuu kuelekea kwenye kivutio hichi. Lakini kiubwa nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti yetu ambayo tunategemea kusoma hivi karibuni tutahakikisha kwamba tutatenga fungu maalumu la kutengeneza miundombinu rafiki katika kituo ama katika kivutio hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la pili nimwambie tu kwamba ipo mikakati kabambe ambayo Serikali na Wizara tumeshaichukua kuhakikisha kwamba tunatunza mazingira katika eneo hili. Tumeshakaa sisi ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii, lakini pia tumeshakaa na watu wa Halmashauri pamoja na TFS kuhakikisha kwamba, la kwanza tunakwenda kupanda miti ya kutosha, lakini tulishatoa maelekezo kwa kuwaambia wananchi waliozunguka maeneo yale kwamba wasifanye shughuli zozote za kibinadamu katika meneo yale, ikiwemo za ufugaji, kilimo na nyingine. Lengo na madhumuni ni ili tutunze kivutio, tuvute watalii lakini pia tuongeze pato, nakushukuru.