Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 315 2023-05-12

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza kugawa maeneo ya kilimo kwa njia ya mnada katika Bonde la Mto Rufiji?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Bonde la Mto Rufiji ni miongoni mwa mabonde 22 ya kimkakati na linakadiriwa kuwa na eneo lenye ukubwa wa hekta 64,896 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bonde hilo ili kujua ukubwa wa eneo na gharama halisi za kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji katika bonde hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, baada ya upembuzi yakinifu kukamilika, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Mkoa wa Pwani, zitaandaa Mpango shirikishi wa namna bora ya ugawaji wa maeneo ya kilimo katika bonde hilo ili kuongeza uzalishaji na tija.