Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza kugawa maeneo ya kilimo kwa njia ya mnada katika Bonde la Mto Rufiji?

Supplementary Question 1

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza: -

Je, ni lini sasa mchakato huu wa Serikali utakwenda kukamilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa maeneo haya ni maeneo ya asili ya makazi ya wananchi, kwa mfano, maeneo ya Mtunda, Moyoyo, Nyafeja Pamoja na Nguwalo.

Je, Serikali ina mkakati gani sasa kuweza kuhakikisha wakati wa kugawa maeneo haya wananchi hawa wanakwenda kupewa kipaumbele, kupata maeneo ya kulima ili waweze kuendesha maisha yao na vilevile kuchangia Pato la Taifa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ni lini mchakato huu unakamilika? Tarehe 23 Mei, 2023 tunategemea taratibu zote za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ziwe zimekamilika na tutaanza ujenzi katika mwaka wa fedha unaoanza 2023/2024, kwa maana kuanzia tarehe 1 Julai mwaka 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili la kuhusu maeneo haya kugaiwa kwa wakazi wa maeneo hayo. Ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba wanufaika wa kwanza wanakuwa ni wakazi wa maeneo hayo. Kwa hiyo nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wake watapata maeneo katika mashamba haya.