Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 24 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 316 2023-05-12

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilaya ya Kilolo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Nancy Hassan Nyalusi, Mbunge Viti Maalum kutoka Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kujenga chuo cha ufundi stadi katika kila mkoa na wilaya nchini. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kujenga vyuo vya ufundi stadi katika wilaya 64 ambazo zilikuwa hazijajengewa vyuo hivyo. Tayari Serikali imeshakamilisha kuandaa michoro na upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Kilolo eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha ufundi stadi ni katika Kijiji cha Luhindo Kata ya Mtitu. Aidha, pamoja na kiasi cha shilingi milioni 45 kilichotolewa awali kwa ajili ya shughuli za maandalizi, tayari Serikali imetuma kiasi cha shilingi milioni 228 kwa kila chuo kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miundombinu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.