Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru Serikali kwa utekelezaji ambao unaendelea. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa vyuo vingi vya VETA vina uhaba wa walimu na vifaa vya kujifunzia;

a) Je, Serikali ina mpamngo gani wa haraka wa kutatua changamoto hiyo?

b) Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba mitaala ya VETA inaendana na shughuli za kiuchumi katika maeneo husika? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nancy, Mbunge Viti Maalum kutoka Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali lake la kwanza, anataka kufahamu kuhusu mkakati wa Serikali kwa upande wa walimu na vifaa. Naomba nilithibitishie Bunge lako Tukufu pamoja na Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeshapata kibali kwa ajili ya kuajiri waalimu 514; na mpaka hivi sasa walimu 151 tayari wameshaajiriwa na kuripoti kwenye vile vyuo ambavyo vilikuwa vinaendesha mafunzo na hivi vyuo vipya; na tutaendelea na mkakati na mchakato huo wa kuajiri walimu kwa kadri fedha zitakavyoruhusu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika swali lake la pili kuhusiana na suala la vifaa vya kufundishia na kujifunzia, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, kwamba Serikali tayari ilishatoa jumla ya shilingi bilioni 8.6 kwa ajili ya ununuzi wa samani kwenye vyuo vile 25 pamoja na vile vya mikoa na vifaa hivyo tayari vimeshanunuliwa na kupelekwa kwenye maeneo hayo. Lakini kwa upande wa vifaa vya kufundishia naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, tarehe 22 mwezi wa nne mpaka tarehe 30 mwezi wa nne, timu yetu ya wataalamu kutoka Wizara ya Elimu ikiongozwa na mimi mwenyewe pamoja na watu wa NACTVET pamoja na VETA tulifanya ziara katika nchi ya China kwa ajili ya kufanya venting ya vifaa vya kujifunzia na kufundishia, na Serikali tayari imetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili kuhusiana na suala la mitaala, naomba nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge tunaendelea na mchakato wa mapitio ya mitaala pamoja na sera yetu ya elimu katika ngazi zote ikiwemo na hii ya VETA. Basi ushauri wake huu wa kuona namna gani tunaweza kuhusisha shughuli za kiuchumi na mitaala yetu tutakwenda kulizingatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.