Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 27 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 355 2023-05-17

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, ni lini majengo yataongezwa katika Chuo cha VETA Urambo ili kuongeza fani ambazo hazitolewi kwa sasa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuongeza baadhi ya majengo yanayokosekana katika Chuo cha VETA cha Urambo ili kuimarisha uwezo na ufanisi wa kutoa mafunzo kwa wananchi wa Urambo yatakayowawezesha kupata ujuzi na kutekeleza shughuli zao za kiuchumi kwa weledi na viwango stahiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetenga fedha kiasi cha shilingi 880,719,315.39 kwa ajili ya kukiimarisha Chuo cha VETA cha Wilaya ya Urambo. Fedha hizi zitatumika katika ujenzi wa miundombinu ya jiko, bwalo la chakula, madarasa na majengo mawili ya karakana. Aidha, ujenzi wa majengo hayo umeanza mwezi Mei, 2023.