Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 364 2023-05-18

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -

Je, lini Serikali itatangaza Mamlaka ya Mji Mdogo Bagamoyo kuwa Halmashauri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Subira Khamis Mgalu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilipokea mapendekezo ya kupandishwa hadhi ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Bagamoyo kuwa Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, baada ya kufanya tathmini ya kina imebainika kuwa, Halmashauri hii bado ina upungufu wa miundombinu mbalimbali yakiwemo majengo ya utawala na huduma za kijamii na mapato yasiyotosheleza kuipandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo kuwa Halmashauri ya Mji.

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuboresha miundombinu katika maeneo ya utawala yaliyopo na siyo kuanzisha maeneo mapya.