Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, lini Serikali itatangaza Mamlaka ya Mji Mdogo Bagamoyo kuwa Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kutokana na Sensa ya Watu na Makazi iliyokuwa imefanyika hivi karibuni, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kuweza kutoa tamko kwamba irudi tu katika mfumo ule wa zamani wa vijiji kuliko hivi sasa kuweza kusubiri kwa sababu imekuwa ni muda mrefu, tangu mwaka 2009?

Swali la pili, pale kwenye Jimbo la Kibiti, Kata za Kibiti, Dimani na Mtawanya ilitangazwa kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo tangu mwaka 2014, shughuli za maendeleo, vikao vya kisheria, mali zimekuwa haziwezi kumilikiwa ipasavyo.

Je, Serikali ina tamko gani kuhusiana na suala hili?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la kwanza la tamko la kurudisha kuwa na vijiji badala ya Mamlaka ya Mji Mdogo. Nirejee kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba vigezo vya kupandisha Mamlaka za Mji Mdogo kuwa Halmashauri za Mji zimewekwa wazi kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa na Mamlaka nyingi za Miji Midogo hizi bado hazijakidhi vigezo hivyo.

Mheshimiwa Spika, kuna Mamlaka za Miji Midogo asilimia 67 ambazo haziwezi kufikia malengo yao wanayojiwekea ya kibajeti na ni asilimia 33 tu ambazo zinafikia malengo yao ya kibajeti kwa asilimia 100, ikiwemo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Bagamoyo. Serikali itaendelea kuliangalia hili na pale tutakapokuwa tumeboresha miundombinu katika maeneo ya kimamlaka yaliyopo sasa tutaendelea kufanya review na kuona ni namna gani tunakwenda kuzipandisha hadhi mamlaka hizi.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la Kibiti. Vivyo hivyo kama nilivyotoa majibu yangu kwenye swali la nyongeza namba moja, kwamba tunaangalia vigezo vya mapato vilevile na kuweza kufanya huduma mbalimbali za kijamii, wao wenyewe kupitia mapato yao ya ndani. Mji Mdogo wa Kibiti tutafanya tathmini kama unakidhi vigezo vile vya kimapato basi tutaona ni namna gani ambavyo unaweza kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo katika Mji wa Kibiti.