Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 28 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 370 2023-05-18

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mbeya – Chunya – Makongolosi – Rungwa – Mkiwa yenye kilometa 503.36 kwa awamu. Sehemu ya Mbeya – Chunya – Makongolosi yenye kilometa 111 ujenzi umekamilika. Ujenzi wa sehemu ya Noranga - Itigi (Mlongoji) kilometa 25 umefikia asilimia 12 na taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi sehemu ya Noranga – Doroto kilometa 6 na Itigi – Mkiwa kilometa 25.6 zimekamilika na Mkataba umesainiwa. Kwa sehemu iliyobaki ya Makongolosi – Rungwa - Noranga kilometa 356 na Mbalizi – Makongolosi kilometa 50 Serikali inaendelea kutafuata fedha kwa ajili ya ujenzi.