Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwanza niseme sijaridhishwa na majibu ya Serikali kwa namna ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyasema. Kwa sababu tarehe 17 mwezi huu, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi akiwa Singida akisaini mikataba aliitaja barabara yetu ya Makongolosi kuelekea Mkiwa kuwa na yenyewe itajengwa kwenye mradi huu wa barabara ambazo amezitaja hapa lakini majibu ya Serikali yanaonekana kugongana.

Mheshimiwa Spika, lakini pamoja na hayo niweze kuuliza sasa. Kwa sababu Mheshimiwa Waziri, alikwishasema fedha zipo za kuweza kujenga zaidi ya kilometa 2300. Je, ni lini sasa Serikali itatoa pesa hizi ili barabara yetu ya Makongolosi kwenda kuunganishwa mpaka Mkiwa iweze kujengwa kwa kuwa barabara hii ni muhimu sana kiuchumi kuunganisha Mkoa wa Mbeya na Singida?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara ya kuanzia Makongolosi kupita mpaka Mkwajuni mpaka Mbalizi ni barabara ya vumbi na imeahidiwa muda mrefu kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami na tayari Serikali imeshatenga kilometa 50 kuweza kujengwa. Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kuanzia Makongolosi hadi Mkwajuni ili iweze kuunganishwa mpaka Mji mdogo wa Mbalizi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Njelu Kasasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Lupa, kwa kufuatilia barabara hii ambayo ni shortcut ya kwenda katika Mkoa wa Mbeya kutokea Mkoa wa Singida.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hii kama nilivyokwisha jibu kwenye majibu yangu ya awali yenye kilometa 503, tumekuwa tukijenga awamu kwa awamu. Pia hadi sasa tumesaini mkataba wa kipande hiki cha Noranga - Doroto kilometa sita na Itigi – Mkiwa kilometa 25.6. Maana yake nini? Maana yake tunaendelea na ujenzi mpaka Makongolosi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, nikuhakikishie ya kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi itaendelea kujenga barabara hii na katika mwaka wa fedha ujao pia tumetenga fedha kwa ajili ya kutoka Makongolosi kwenda Singida.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, barabara ya Makongolosi – Mbalizi. Barabara hii imekuwa ikitengewa fedha kila mwaka na mwaka huu imetengewa kilometa 50 na mwaka ujao pia tumewekea fedha za kuanza ujenzi wa barabara hii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mbunge kwamba barabara hii katika mwaka ujao wa fedha itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante sana.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Majita – Musoma – Busekela yenye urefu wa kilometa 92 imechukua muda mrefu sana kukamilika. Hadi sasa imekwishajengwa kwa kilometa tano tu.

Je, Serikali ni lini ina mpango wa kupeleka fedha za kumalizia barabra hiyo ukizingatia itaongeza au kukuza uchumi kwa wana Musoma Vijijini na Mkoa wa Mara kwa Ujumla?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa, Agnes Marwa, kuhusiana na suala la barabara hii ya Majita – Musoma. Ni kweli tumekwishajenga kilometa tano na suala la kupeleka fedha tutaendelea kupeleka fedha katika barabara hii ili ikamilike kwa ukamilifu wake, ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na foleni inayotokana kati ya Mkoa wa Morogoro na Pwani. Ni lini ujenzi wa barabara nne kuanzia Chalinze mpaka Morogoro Mjini utajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ya Chalinze kwenda Morogoro ni barabara ambayo tumeifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kupitia makampuni ya Korea Kusini na mwezi wa nne walileta ripoti maalum inayoonesha ni kwa kiwango gani tujenge. Je, iwe ni kwa mfumo wa PPP ama iwe ktika mfumo wa EPC + Financing? Sasa Serikali imeona umuhimu wa barabara hii iwe katika mfumo wa PPP. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge niwahakikishie na wananchi wote wa eneo hilo kwa sababu ni barabara kuu, kwamba barabara hii itajengwa kwa mfumo wa PPP na tayari tumeshaanza ku– engage na wakandarasi, ahsante.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 4

MHE. ALILY A. MLAGHILA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya Uyole – Kasumulu ina zaidi ya miaka 35 sasa, muda ambao imekwishapita design age yake. Je, Serikali haioni sasa ni wakati sahihi wa kuanza kuiwekea hata layer ya juu badala ya kusubiri ibomoke yote?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Jumbe, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kwa kufuatilia barabara hii na nimhakikishie tu kwamba kwa kuwa hapa Kasumulu ni lango muhimu la kwenda katika Nchi Jirani ya Malawi. Katika bajeti zetu za TANROADS kupitia Mkoa wa Mbeya tumetenga fedha kwa ajili ya kuboresha barabara hii iweze kupitia wakati wote, ahsante.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 5

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. nilitaka kuuliza swali la nyongeza kwamba barabara itokayo Malagarasi kwenda Uvinza, kipande cha kilometa 51 kimekuwa na muda mrefu sana na sasa kimeanza kutengenezwa lakini kinasuasua sana.

Nini mpango wa Serikali kuhakikisha wanamaliza maana barabara hiyo ni kipande hicho ndicho kilichobaki?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, Mbunge wa Kigoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kati ya maeneo ambayo barabara imechukua muda mrefu ni pamoja na kipande hiki
cha Malagarasi – Uvinza ili Mkoa wa Kigoma uweze kuunganishwa na mikoa jirani ikiwemo Tabora.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wote wa Kigoma. Mtakumbuka ziara aliyoifanya Mheshimiwa Rais, alipokuwa Kigoma ni miongoni mwa barabara hizi ambazo alizotoa maelekezo kwamba ni lazima ikamilike. Sisi Wizara ya Ujenzi katika bajeti hii inayoendelea na inayokuja tumetenga fedha kuhakikisha kwamba barabara hii inakamilika, ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 6

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru Serikali kwa barabara yetu ya Kiberashi – Handeni – Chemba hadi Singida lakini ili barabara hiyo iweze kutumika vizuri kuna interchange mbili. Kwanza ni kutoka Zamahelo mpaka Donsee nyingine ni kutoka Goima hadi Bicha. Sasa nataka kujua mkakati wa Serikali wa kuhakikisha interchange hizo zinajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Monni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pongezi za Serikali nazipokea kwa niaba lakini pongezi hizi ziende kwa Mheshimiwa Rais, maana yeye ndiye anayetoa hizi fedha na hususani katika ujenzi wa barabara hii ambayo Mheshimiwa Mbunge umeizungumzia. Kwa kuanzia kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii nafikiri itakuwa vema zaidi tukianza kama ambavyo Serikali imepanga ndipo tuanze na hizo zingine kwa kuwa hii ndio itakuwa lango muhimu

la kuunganisha kati ya Mkoa wa Dodoma na Mkoa jirani, ahsante.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 7

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Mpanda – Kaliua – Ulyankulu mpaka Kahama yenye urefu wa kilometa 472 iko kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015/2020 lakini iko kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025. Je, barabara hii sasa ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya kilometa 472 ni kweli iko kwenye Ilani ya 2025 na Serikali ya Chama cha Mapinduzi inatekeleza ilani hii ya 2025. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba kwa kuwa bado tunaendelea na utekelezaji wa ilani hii, uwe na uhakika kwamba pia barabara yako itajengwa.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara inayounganisha Mikoa ya Mbeya, Tabora na Singida inayoanzia Makongolosi hadi Rungwa?

Supplementary Question 8

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi. Ipo barabara ya kutoka Mbezi kwenda Mpiji Magohe au barabara ya Victoria Road. Ni barabara ambayo iko ndani ya mpango kwa miaka mingi na bajeti lakini iko chini ya ahadi ya Mheshimiwa Rais lakini ndani ya ilani kwa miaka 10. Ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Mtemvu, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii iko kwenye Ilani lakini pia tumekwisha ifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na katika bajeti ijayo nikuombe Mheshimiwa Mbunge tutakayoisoma jumatatu na jumanne, tuipitishe bajeti hiyo ili barabara hii iweze kujengwa kwa kuwa ni miongoni mwa barabara hizo pia, ahsante.