Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 387 2023-05-22

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi wa Kilimanjaro kwa kumalizia ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 na 2022/2023, Serikali ilitenga shilingi bilioni 1.96 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 37 katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga shilingi bilioni 2.35 kwa ajili ya ujenzi na ukamilishaji wa vituo vya afya vitatu na zahanti 17.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya vituo vya afya na zahanati nchini kote.