Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, lini Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi wa Kilimanjaro kwa kumalizia ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na maswali mazuri sana na Serikali lakini nilitaka kujua, je, ni lini katika ajira hizi zilizotangazwa watumishi hawa wataingia kazini ili waende wakawatibu Watanzania wengi ambao wanahitaji huduma hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira hizi zilizotzngazwa zote 21,300 katika sekta ya elimu na afya zitaanza kutumika au wataingia kazini baada ya mchakato wa ajira hizi kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo muda siyo mrefu Mheshimiwa Malleko kule Kilimanjaro lakini na Waheshimiwa Wabunge wote hapa wataanza kuona wale watumishi wapya wanaaanza kwenda kwenye maeneo yao.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, lini Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi wa Kilimanjaro kwa kumalizia ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kuna jitihada nyingi katika Jimbo la Serengeti Kijiji cha Nyamatale pale Nyirongwa wamejenga boma, pale Kitalahota Kitongoji katika Kijiji cha Nyamakobiti, pia wamejenga boma kwa jajili ya zahanati, Kijiji cha Bisalala, Ngalawani na Kenokwi.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa mchango wake kusaidia jitihada hizi za wananchi kukamilisha zahanati hizi? ahsante

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amsabi la zahanati hizi za vijiji ambavyo amevitaja Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi hawa kadri ya upatikanaji wa fedha. Na tutajitahidi, kwa sababu ni adhma ya Serikali hii ya awamu ya sita kuhakikisha afya za Watanzania zinaimarika zaidi kwa kupata huduma iliyobora. Tutahakikisha kadri ya upatikanaji wa fedha tunachangia nguvu za wananchi wa pale.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, lini Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi wa Kilimanjaro kwa kumalizia ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Rungwe Mheshimiwa Mbunge wa jimbo pamoja na Diwani wa Kata ya Kiwila na wananchi wameweza kujenga Zahanati ya Kiwila lakini bado haijamalizika.

Je, ni lini, Serikali mtaenda kuweka nguvu ili tuweze kumaliza zahanati ile?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Zahanati hii ya Kiwila kule Rungwe itatengewa fedha kadri ya upatikanaji wa fedha; na tutaangalia katika mwaka wa fedha huu 2023/2024 ambao tunaenda kuanza kuutekeleza kama imetengewa fedha. Kama haijatengewa fedha tutaangalia kuitengea fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza: - Je, lini Serikali itaunga mkono jitihada za wananchi wa Kilimanjaro kwa kumalizia ujenzi wa maboma ya zahanati na vituo vya afya?

Supplementary Question 4

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi. Katika Jimbo la Momba kuna vijiji zaidi ya 20 ambavyo wananchi wamejenga maboma na wanahitaji kuungwa mkono na Serikali. Mfano, Kijiji cha Mwenehemba, Mamsinde one, Namsinde two, Kakozi, Chilangu na vinginevyo.

Je, ni lini, Serikali itatusaidia ili kumalizia maboma haya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itasaidia umalizaji wa maboma haya 20 aliyotaja Mheshimiwa Condester Sichalwe kadri ya upatikanaji wa fedha. Nitumie nafasi hii kuwataka Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini kuhakikisha wanatenga fedha katika mapato yao ya ndani kuunga mkono juhudi za wananchi katika maeneo yao ya kiutawala ili kuweza kumalizia iwe ni katika zahanati iwe ni katika shule.