Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 388 2023-05-22

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo ilikuwa na upungufu wa watendaji wa vijiji 33. Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 na 2022/2023 Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Biharamuro imeajiri watendaji wa vijiji 20.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Biharamuro imeomba kibali cha kuajiri watendaji wa kata saba na watendaji wa vijiji 13.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendela kuajiri watendaji wa vijiji na kata katika halmashauri zote inchini iliwemo Halmashauri ya Wilaya ya Biharamuro kadri ya bajeti itakavyoruhusu.