Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Biharamulo kijiografia ni eneo kubwa sana na tumekuwa katika scarcity hiyo ya watendaji kwa muda mrefu sana. Sasa kwa sababu umesema tayari maombi yetu mnayo.

Swali la kwanza; je, ni nili tutapatiwa kibali tuweze kuajiri watendaji ku-cover zile nafasi ambazo zimebaki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili kama unavyojua Wilaya ya Biharamulo sasa population yetu ni watu 457,114. Jimbo hili ndilo linaloongoza kwa idadi kubwa ya watu kwa Mkoa wa Kagera, lakini kijiografia pia ni Jimbo kubwa zaidi lina vijiji 79, kata 17 lakini zilizotawanyika sana.

Je, huoni kwamba iko haja ya Serikali kutupatia usafiri kwa ajili ya watendaji wa vijiji na kata ili huduma za wananchi ziweze kufika kwa haraka zaidi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la kwanza la Mheshimiwa Ezra Chiwelesa, la lini kibali hiki cha ajira. Nikirejea majibu yangu ya msingi, tutatoa vibali hivi kadri ya bajeti itakavyoruhusu, lakini tayari Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo imeshapata watendaji wa vijiji 20 katika mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023. Kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge Serikali inatambua upungufu huu na inaendelea kulifanyia kazi na muda si mrefu mtaona watendaji hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la usafiri. Wote humu ndani ni mashahidi katika awamu hii ya sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kwa mara ya kwanza kuanza kutoa pikipiki kwa watendaji wa kata zetu zote nchini. Tayari walikuja Dodoma hapa na wakakabidhiwa pikipiki hizo. Na zile kata ambazo bado zimesalia kuna baadhi ya Wakurugenzi ambao wameanza kununua kwa mapato yao ya ndani na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wetu. Kwa hiyo niwatake tena Wakurugenzi wa Halmashauri kote nchini kuhakikisha wanatenga fedha ya kununua usafiri kwa ajili ya watendaji wa kata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na inaporuhusu bajeti basi hadi kwa watendaji wa vijiji, lakini mpaka sasa Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kupunguza upungufu huu wa usafiri.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika Mkoa wa Arusha kuna watendaji wa vijiji wengi wamekuwa wakikaimu. Mfano tu, katika Wilaya ya Longido kuna watendaji wa vijiji 23 wamekaimu kwa muda mrefu na wana sifa.

Je, ni lini Serikali itatoa ajira kwa watendaji wa vijiji hawa? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itatoa ajira za watendaji wa vijiji kadri ya bajeti itakavyoruhusu. Niseme tu, kukaimu utendaji wa kijiji huu, hawa 23 hai-guarantee kwamba ajira zitakapotangazwa kwamba wao ndi wataingia, zitafuata mchakato kama inavyotaka kwa ushindani na wale ambao wataonekana wana sifa za kuajiriwa ndio ambao wataajiriwa na kuwa watendaji wa vijiji. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge avute subira na kadri ya bajeti itakavyoruhusu Serikali itaajiri.

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 3

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Jimbo la Nachingwea lina kata 36, kati ya hizo kata mbili hazina watendaji wa kata, lakini lina vijiji 127 na vijiji 37 havina watendaji wa vijiji. Na kwa kuwa tunajua watendaji hawa ndio wanaosukuma shughuli zote za maendeleo katika maeneo yetu;

Je, ni lini Serikali itatoa vibali kwa ajili ya kupata hawa watendaji ambao watatusaidia kwenye maendeleo kwenye maeneo yetu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kata mbili ambazo hazina watendaji na vijiji 37 ambavyo havina watendaji kule Nachingwea ni adhma ya Serikali kuhakikisha kwamba kila kata, kila kijiji kina watendaji. Kadri ya bajeti itakavuoruhusu basi viabali hivi vitaendelea kutolewa. Na nikutaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko mbioni kuajiri watendaji wa kata katika kata zote ambazo ziko wazi nchini. Kwa hiyo ni kuvuta Subira, nikuhakikishie kwamba hilo linafanyiwa kazi.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 4

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan analeta fedha nyingi sana za miradi katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara, na kwa kuwa miradi hiyo mingi haiendi vizuri na sababu moja wapo ni kukosekana kwa mtumishi Mkuu wa Idara ya Ujenzi;

Je, ni lini Serikali inapeleka injinia mzoefu wa majengo ya ujenzi Halmashauri ya Mji wa Ifakara ili kunusuru miradi hii?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiajiri mainjinia, kulitokea changamoto ya kuwa na upungufu wa mainjinia katika halmashauri zetu nchini, baada ya kuanzishwa TARURA; mainjinia wengi wa halmashauri walihamia wakala wa TARURA. Mwaka wa fedha uliopita Serikali iliajiri mainjinia zaidi ya 265 ambapo kila halmashauri nchini ilipata injinia mmoja, na hivi sasa Serikali ipo katika mchakato wa kuajiri tena mainjinia kwa ajili ya kutoa upungufu huu ambao upo ikiwemo kule kwa Mheshimiwa Asenga na tutaangalia pale ambapo ajira hizi zitapatikana basi kule kwa Mheshimiwa Asinga nao watapata injinia.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa kibali cha ajira za watendaji wa kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 5

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Halmashaui ya Wilaya ya Rorya ni mwaka wa tatu sasa haijawahi kuajiri watendaji wa vijiji wala wa kata na kwa kuwa sasa tumeomba kibali kwa ajili ya kupata kuajiri watendaji hawa;

Je, Serikali inachelewa nini kutupa kibali na sisi tuweze kuajiri kwenye maeneo ambayo yana upungufu wa watendaji wa vijiji na watendaji wa kata?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itatoa vibali hivi vya ajira kadri ya bajeti itakavyoruhusu, na tutaangalia katika bajeti iliyotengwa mwaka 2023/2024, kama kuna nafasi hizi zilizotangazwa basi kule Rorya ambapo kuna upungufu na wameomba kibali, kibali kiweze kutolewa. Kama hakuna iliyotengwa basi tutaipa kipaumbele katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.