Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 392 2023-05-22

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

Je, kwa namna gani Serikali inatekeleza Kanuni ya Kimtandao ya Network Neutrality katika utoaji na upatikanaji wa huduma za jamii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya Network Neutrality ni hali ya kuweka usawa katika huduma zote zinazopatikana kwenye mtandao wa intaneti bila kuathiri kasi, gharama wala upendeleo wa tovuti fulani au maudhui ya aina fulani mtandaoni. Serikali inasimamia Sekta ya Mawasiliano kwa kuzingatia kikamilifu Kanuni ya Kimtandao ya Network Neutrality ambapo mtoa huduma yeyote wa mtandao wa intaneti anaruhusiwa kutoa huduma ya mtandao kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa. Aidha, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeweka utaratibu wa kuwezesha watoa huduma kutoza gharama za data bila kujali ni ya matumizi ya mitandao gani ya kijamii, tovuti au programu tumizi mbalimbali.