Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, kwa namna gani Serikali inatekeleza Kanuni ya Kimtandao ya Network Neutrality katika utoaji na upatikanaji wa huduma za jamii?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa, tunafahamu kwamba, Serikali inatumia e-Government na TEHAMA kwa ajili ya kutoa huduma za kijamii kiserikali, lakini mara kadhaa wananchi wamekuwa wakikosa huduma kwenye ofisi za Serikali kwa sababu ya kwamba, mtandao uko chini. Ni kwa nini sasa Serikali isije na mkakati mahususi wa kuhakikisha kwamba, utolewaji wa huduma kwa kutumia e-Government na TEHAMA kwenye ofisi za Serikali unatengenezewa upekee na kuhakikisha kwamba, wananchi hawakosi huduma kwa sababu za mtandao uko chini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, tumekuwa tunaona Serikali inafanya udhibiti wa mitandao, hususan katika kipindi cha uchaguzi, lakini pia tunafahamu kwamba, sasa hivi Serikali inachagiza uchumi wa kidijitali na wananchi wengi wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuhakikisha wanafanya shughuli zao za kiuchumi. Ni kwa nini sasa Serikali isione umuhimu wa kuhakikisha kwamba, majukwaa haya ya mitandaoni hayakosi mawasiliano, hususan kipindi ambacho Serikali inafanya udhibiti wa kasi hususan kipindi cha uchaguzi?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA WIZARA YA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza kuhusu matumizi ya internet katika ofisi za Serikali. Serikali imewekeza katika miundombinu, Ujenzi wa Mkongo wa Taifa. Katika ujenzi huo tuna capacity mbalimbali, tuna kitu kinaitwa Synchronize Transport Module maana yake STMA. Hizi STM kuna 1, 2 na 3; 1, 2, 3, 4 maana yake kwamba, ni capacity na speed ambapo kwa mfano STM 1 ambayo ina MBPS 155 maana yake hiyo ni capacity yake, lakini kuna ya 491, kuna ya 2488, lakini sasa niombe na kuwashauri wataalam wa eGA na wataalam ambao wako katika Wizara mbalimbali, wafanye tathmini ya mahitaji halisi ili waweze kujua kwamba, wanaweza wakapata capacity ipi itakayoendana na traffic wakati wanapokuwa wanahudumia wananchi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipengele cha pili cha udhibiti. Kuna Profesa mmoja anaitwa Tim Wu kutoka Colombia Law School alisema kwamba, ili ubunifu uendelee na ili tuwe na freedom ya access to information na ili business na innovation zizidi kukua ni lazima tusiweke restrictions katika aina gani ya mtandao tuweze ku-access na aina gani ya contents tuweze ku- access.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali yetu kupitia TCRA tumeweka utaratibu kwa watoa huduma kuhakikisha kwamba hakuna restriction ya aina ya content ambayo mwananchi anaweza kui-access.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.