Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Water and Irrigation Wizara ya Maji 394 2023-05-22

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga miradi ya maji katika Vijiji vya Mateka, Tukuzi, Kitelea na Sepukila Wilayani Mbinga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani Mbinga ambapo kwa Vijiji vya Kitelea na Sepukila utekelezaji wa miradi ya maji unaendelea na utakamilika mwezi Juni, 2023. Aidha, kwa Kijiji cha Tukuzi usanifu umekamilika na kwa Kijiji cha Mateka usanifu utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024 na ujenzi wa miradi ya maji kwenye vijiji hivyo utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024.