Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miradi ya maji katika Vijiji vya Mateka, Tukuzi, Kitelea na Sepukila Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kuishukuru Serikali kwa kuanza kutekeleza miradi katika Vijiji vya Sepukila na Kitelea pia kuandaa kutekeleza miradi ya maji katika Vijiji vya Tukuzi na Mateka. Vijiji vya Nzokai, Kilimani, Rudisha, Mikolola na Njomlole vina changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji. Nataka nijue sasa ni lini Serikali itaandaa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi kwenye maeneo haya. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipokee shukrani zake kwa Serikali, lakini zote ni jitihada zake za ufuatiliaji wa karibu na ushirikiano wake mzuri ndani ya Wizara yetu ta Maji. Mheshimiwa Mbunge, nawe tunakupongeza katika hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji hivi alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge tayari vipo katika hatua mbalimbali za kuona kwamba na vyenyewe tunavifikishia maji safi na salama bombani. Hivyo, katika mwaka ujao wa fedha, vijiji hivi navyo tutavigusa katika namna ya kuona huduma inapelekwa.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miradi ya maji katika Vijiji vya Mateka, Tukuzi, Kitelea na Sepukila Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kujua katika bajeti ya mwaka 2022/2023, Serikali iliahidi kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Jimbo la Bunda. Je, ni lini ahadi hii itatimizwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tayari mradi ambao unatarajiwa kupelekwa Bunda umefikia hatua nzuri, Mhandisi
Mshauri yuko site. Mheshimiwa Mbunge nakupongeza kwa kufuatilia, kama tulivyoongea wiki iliyopita ofisini, tayari Mhandisi Mshauri anakamilisha na wiki hii tunamtarajia arejeshe taarifa ya kuona tathmini ya thamani ya mradi ambao tutakwenda kuujenga.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miradi ya maji katika Vijiji vya Mateka, Tukuzi, Kitelea na Sepukila Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ninapenda kufahamu kwenye Vijiji vya Mpanyani Shule ya Sekondari, Huria, Chiroro, Masiku pamoja na Namichi tayari pameshachimbwa visima virefu. Je, ni lini sasa Serikali iko tayari kuweka pampu kwenye maeneo haya ili wananchi waweze kupata maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji hivi alivyovitaja vyote tunatarajia viweze kuendelezwa visima vilivyochimbwa. Tumshukuru Mheshimiwa Rais tumeendelea kupata fedha za P4R, Mikoa yote itapelekwa fedha, kwa hiyo tunatarajia sasa distribution itakwenda kufanyika na wananchi wataanza kunufaika na visima vilivyochimbwa.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga miradi ya maji katika Vijiji vya Mateka, Tukuzi, Kitelea na Sepukila Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Mradi mkubwa wa maji uliogharimu takribani shilingiza bilioni 520 za Kitanzania kule Arusha sasa hivi karibu unamalizika. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu ya kusambaza maji katika vijiji ambavyo bomba kuu limepita?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mradi huu tuko mwishoni kabisa na tayari vijiji vingi vimenufaika, tayari maji haya kutoka kwenye mradi yameingizwa kwenye laini ambazo zina-exist. Vilevile maeneo yote ya vijiji hivyo alivyovitaja na vingine vyote ambavyo vimepitiwa na bomba kuu vinakwenda kupata huduma ya maji safi na salama.