Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 30 Water and Irrigation Wizara ya Maji 395 2023-05-22

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Mji Mdogo Gairo watapata maji ya kutosha?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua tatizo la maji linaloukabili Mji wa Gairo na jitihada zinaendelea kuchukuliwa ili kupunguza adha ya maji kwa wakazi wa Mji huo. Jitihada zinazofanyika ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu viwili na sasa mkandarasi yupo eneo la mradi anaendelea na kazi. Vilevile, Serikali itafanya ukarabati wa mradi wa maji ya mserereko Gairo, Mkandarasi ameajiriwa na kazi inayoendelea ni mapitio ya mradi na ujenzi utaanza mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa muda mrefu ni kutumia chanzo cha Mto Chagongwe utakaohudumia wananchi wa Mji wa Gairo na kwa sasa Wizara inaendelea kufanya usanifu na ujenzi utafanyika katika Mwaka wa Fedha 2023/2024.