Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Mji Mdogo Gairo watapata maji ya kutosha?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, hasa kwa mradi wa Chagongwe kusikia kuwa utaanza. Licha ya hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata 29 za Manispaa ya Morogoro zinapata maji ya mgao. Je, kuna mkakati gani wa kupata maji safi na salama kila siku kwenye Kata hizo 29 za Manispaa ya Morogoro? (Makofi)

Swali la pili, mradi wa Magadu ambao upo kwenye Manispaa ya Morogoro umechukua muda mrefu na haujakamilika; je, ni lini utakamilika na kuanza kutoa maji kwa wananchi kwenye Kata hizo zinazozunguka? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kwenye maeneo yote ya Mji wa Morogoro tuna mradi mkubwa wa AFD ambao tunatarajia ukaongeze uzalishaji wa maji na tatizo hili la mgao mkali wa maji pale Morogoro tunatarajia litapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mradi wa Magadu tayari tumeutekeleza kwa asilimia 90, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulishaongea pamoja hili na tumefuatilia kwa pamoja Wakandarasi wanaendelea na kazi na tayari Wizara tumeshapeleka fedha, tunatarajia kufika mwezi Juni huu mradi wa Magadu nao uanze kutoa huduma kwa wananchi. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Mji Mdogo Gairo watapata maji ya kutosha?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilio cha maji safi na salama Tanzania ni kama wimbo wa Taifa na wanaoteseka zaidi ni wanawake. Sasa hivi tunavyoongea ni masika na maji yanapotea na hakuna kinachoendelea kutoka Serikalini.

Je, ni lini sasa Serikali itatumia kuvuna maji haya ya mvua kuwaponya wanawake wa Makanya, Hedaru, Hundugai, Ngoyoni na Holili kule Kilimanjaro? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ni tabia ya maji ya mvua kupotea, lakini sasa hivi Wizara tumejipanga kujenga mabwawa maeneo yote ambayo yamekuwa na mafuriko na maji yanapotea kuelekea baharini. Tutachimba mabwawa Mheshimiwa Mbunge na tayari mitambo tunayo. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu fedha nyingi kutumika kuleta mitambo mikubwa mitano ya kuchimbia mabwawa.