Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 32 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 416 2023-05-24

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, lini Barabara ya Majengo – Ruvuma – Subira - Muungano itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaanza mipango ya ujenzi wa Barabara ya Majengo – Ruvuma - Subira na Muungano kwa kiwango cha lami ambapo katika Mwaka wa Fedha wa 2023/2024, jumla ya shilingi milioni 517.50 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami nyepesi kilomita moja.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha.