Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini Barabara ya Majengo – Ruvuma – Subira - Muungano itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri yenye matumaini ya Serikali, eneo husika lina umbali wa takribani kilometa 10. Je, Serikali inatoa commitment gani ya kumaliza kilometa tisa zilizobaki?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imeazimiwa kujengwa kilometa 20 kwa lami kwa mpango wa TACTIC. Je, lini ujenzi huo utaanza?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza, hii commitment ya fedha kwa barabara kilometa zilizosalia. Kwanza, barabara hii ina jumla ya kilometa 9.5 na tayari katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali ilitenga shilingi milioni 270 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili, vilevile kuhakikisha kwamba mifereji ya maji kilometa mbili inajengwa.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba Serikali imetenga hiyo kilometa moja kwa shilingi milioni 517, tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, tayari Mheshimiwa Mbunge mwenyewe, Mheshimiwa Msongozi, lakini vilevile Mheshimiwa Dkt. Ndumbaro, Mbunge wa Jimbo pale naye amekuwa akiifuatilia sana barabara hii; Mheshimiwa Nyoka, Mheshimiwa Judith Kapinga, wote walikuwa wakifuatilia sana barabara hii na tutaendelea kuitafutia fedha kama Serikali ili kuweza kuhakikisha kilometa zote 9.5 zinakwisha.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali la pili la kilometa 20 za Nanyamba kule Mkoani Mtwara. Mradi huu wa TACTIC hivi sasa upo katika kupata wale wakandarasi ambao watajenga barabara za TACTIC hapa nchini. Tayari timu zile za evaluation zilishakaa kule Jijini Arusha kuhakikisha kwamba tunapata wakandarasi wenye uwezo wa kukamilisha mradi huu. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Chikota kwamba muda si mrefu mradi huu utaanza.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini Barabara ya Majengo – Ruvuma – Subira - Muungano itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Tunaishukuru Serikali kwa kuanza ujenzi wa kilometa 600 za lami kutoka Benki ya CRDB pale Mjini Mugumu kuelekea Hospitali ya Wilaya. Pamoja na ujezni huu barabara hii imesimama sasa kwa muda, na kwa vile inaelekea hospitali ya wilaya, imekuwa na usumbufu mkubwa sana kwa wananchi. Pamoja na jitihada nyingi za mawasiliano na TARURA, wilaya na mkoa bado ujenzi huu hauendelei. Je, ni lini changamoto hizi zitatatuliwa na ujenzi ule ukamilike? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii anayozungumzia Mheshimiwa Mrimi ya CRDB – Hospitali katika Mji wa Mugumu imekuwa na changamoto ya mkandarasi mwenyewe kuwa anafanya kazi kwa taratibu sana. Mkandarasi huyu ameshaitwa kwenye Kamati mbalimbali za pale katika Wilaya ya Serengeti kuangalia ni namna gani anaweza akamaliza barabara hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tukitoka hapa tutakaa naye tuweze kuona tunaweka mkakati gani na Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Mara na Meneja wa TARURA wa Wilaya ya Serengeti kuona mkandarasi huyu anarudi site vipi kwa haraka sana kumalizia barabara hii.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini Barabara ya Majengo – Ruvuma – Subira - Muungano itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itajenga barabara ya Mijengweni – Shiri Njoro, kilometa 15 tu? Barabara hii ni muhimu sana kwa kusafirisha mazao ya wananchi, lakini wananchi kuja kupata huduma huku Bomang’ombe.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Mijengweni itajengwa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha, lakini Mheshimiwa Mbunge ni shahidi kwa jitihada za Serikali ambazo zimefanyika katika Wilaya ya Hai, tayari kupitia TARURA tumejenga Barabara ya Nyerere yenye mita 600; tumejenga Barabara ya Stendi – TTCL kwenda RC Church; tumejenga Barabara ya Bomang’ombe pale na tunaendelea. Kuna barabara nne kwa jitihada zake ambazo zinaendelea kujengwa na tutatafuta fedha kwa ajili ya kujenga hizi kilometa 15 kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameomba.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini Barabara ya Majengo – Ruvuma – Subira - Muungano itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Swali langu ni hili hili nalirudia kila wakati. Ile bypass road kutoka Chekereni kwenda Kahe – Mabogini na TPC wataifanya nini au wana mkakati gani kwa sababu hii iko kwenye Ilani na ahadi za viongozi wetu wakubwa? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika bypass road hii Serikali inaifanyia kazi kupitia Wakala wa Tanzania ambao ni TANROADS na tutakaa pamoja na wenzetu wa TANROAD kuona mipango yao ni ipi kuhakikisha barabara hii inatekelezwa kama Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambavyo ilielekeza.