Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 34 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 446 2023-05-26

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapitia upya mipaka na kuweka alama za Hifadhi katika Vijiji vya Ndongosi, Mtunduaro, Litumbandyosi na Kiwombi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vya Ndongosi, Mtunduaro, Litumbandyosi na Kiwombi vinapakana na Hifadhi ya Msitu wa Litumbandyosi katika Wilaya ya Mbinga. Kwa sasa Serikali inaendelea na utaratibu wa kuhakiki msitu huo wa Hifadhi wa Litumbandyosi kwa kuwashirikisha wananchi, baada ya kukamilika kwa uhakiki huo zitawekwa alama za mipaka zinazoonekana ili kuwezesha wananchi kutambua eneo la hifadhi na hivyo kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza kutokana na kutokuwepo kwa mipaka inayoonekana wazi.