Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 26 2016-09-07

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa mipaka kati ya TANAPA na vijiji na vitongoji jirani vinavyowazunguka.Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza mgogoro huu kati ya TANAPA na vitongoji vya Kitame, Razaba, Gama-Makani katika Kata ya Makurunge?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro yote mitatu iliyotajwa na Mheshimiwa Mbunge inahusiana na hifadhi ya Taifa Saadani iliyoanzishwa kisheria kwa Tangazo la Serikali Namba 281 la mwaka 2005.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro baina ya Kitongoji cha Kitame, Kijiji cha Makurunge na hifadhi umetokana na malalamiko kwamba wananchi hawakushirikishwa katika zoezi la uwekaji wa mipaka hivyo kusababisha yaliyokuwa maeneo yao kuingizwa ndani ya hifadhi bila ridhaa yao. Hata hivyo, kumbukumbu zinaonyesha kwamba kuwa wananchi walishikikishwa kikamilifu kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa mkutano wa kijiji mama cha Makurunge ambacho kitongoji hiki ni sehemu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro baina ya shamba la Razaba na hifadhi umetokana na utata wa takribani eneo la hekta 3,441 alilopewa mwekezaji Bagamoyo Eco-Energy kwa hati miliki namba 123097 ya terehe 9 Mei, 2013 ili amiliki na kuendesha shughuli za kilimo cha miwa katika eneno ambalo kiuhalisia limo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Saadani. Juhudi za kutatua mgogoro huu ziliendelea kufanyika kwa takribani miaka minne kwa kuhusisha ngazi za Vijiji, Wilaya, Mkoa na Wizara zinazohusika na hatimaye kutolewa maelekezo kupitia agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu agizo ambalo lilizingatia athari za mazingira zilizotishia uwepo wa hifadhi ya Saadani iwapo kilimo cha miwa kingeruhusiwa katika eneo linalozungumziwa.
Mgogoro baina ya Gama -Makani na hifadhi unatokana na malalamiko ya wananchi kuwa baadhi ya waliofidiwa wakati wa uanzishwaji wa hifadhi katika eneo hilo hawakuwa wamiliki wazawa wa maeneo hayo. Hata hivyo taarifa zinaonyesha kuwa mchakato wa malipo ya fidia ulifuata taratibu muhimu ikiwemo ushirikishwaji wa karibu wa uongozi wa Wilaya ya Bagamoyo, Serikali za Kata na Serikali za Vijiji husika ambao ulizingatia ilivyohitaji la kuwalipa wananchi waliostahili na si vinginevyo. Pamoja na maelezo haya, Serikali imekwishaunda timu ya pamoja ya wataalam ambayo inaendelea na kazi ya kutafuta suluhisho la migogoro ya ardhi nchini ikishirikisha Wizara mbalimbali kama ilivyoahidiwa wakati wa Bunge la Bajeti lililoahirishwa mwezi Juni, 2016.