Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 77 2023-09-05

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:-

Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha mabasi cha kisasa katika Halmashauri ya Wilaya Tunduru?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru iliwasilisha andiko la mradi wa ujenzi wa kituo cha mabasi. Baada ya kuchambuliwa andiko hilo halikukidhi vigezo hivyo lilirejeshwa Halmashauri kwa ajili ya kufanya maboresho na kuanza kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo ya mabasi limekodishwa kwa Kampuni ya Kalpataru Power Transmissions Ltd inayofanya kazi ya ujenzi wa gridi ya Taifa kwa miaka miwili, (2022/2023 na 2023/2024). Hivyo, Ofisi ya Rais TAMISEMI inaielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kukamilisha tathmini ya gharama za mradi na kuanza kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo katika mwaka wa fedha 2024/2025, ahsante.