Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha mabasi cha kisasa katika Halmashauri ya Wilaya Tunduru?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza naomba kuchukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa majibu mazuri yanayoonyesha nia na mkakati wa kuanza mradi ule, lakini bado nina swali dogo la nyongeza. Je, Naibu Waziri yuko tayari kutembelea eneo la mradi ili kujionea umuhimu au ukubwa wa uhitaji wa mradi huo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza nipokee pongezi zake kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa iliyoifanya katika ujenzi wa vituo vya mabasi nchini kote. Nimhakikishie tu Mheshimiwa kwamba niko tayari baada ya kumaliza shughuli za Bunge, tutakubaliana baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu tupange ratiba ya kwenda Tunduru tukapitie pale.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha mabasi cha kisasa katika Halmashauri ya Wilaya Tunduru?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itajenga stendi ya mabasi katika Jimbo la Muhambwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Muhambwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawaelekeza Halmashauri ya Kibondo kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi na kuanza kutenga mapato ya ndani. Lakini kama uwezo hautatosha walete andiko hilo Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kutafuta fedha za kujengea stendi hiyo.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha mabasi cha kisasa katika Halmashauri ya Wilaya Tunduru?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Momba hatuna stendi hata moja na kuna uhitaji mkubwa; je, ni lini Serikali itatupatia fedha tuweze kujenga kituo cha mabasi ili kitumike kama chanzo cha mapato kwenye Halmashauri yetu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni wajibu wa Wakurugenzi wa Halmashauri kutambua maeneo kwa ajili ya huduma za kijamii ikiwemo stendi, pia, ni wajibu wao kuanza kutenga fedha kupitia mapato ya ndani na kuwasilisha maandiko Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi huo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa tunatoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Momba kufanya tathmini ili tujue gharama zinazohitajika ili waanze kutenga mapato ya ndani lakini pia ofisi ya Rais TAMISEMI tuone uwezekano wa kupata fedha kwa ajili ya shughuli hiyo, ahsante.