Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 84 2023-09-05

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka huduma ya maji ya DAWASA katika Kata za Buza, Vituka, Makangarawe na Sandali - Temeke?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy George Kilave, Mbunge wa Jimbo la Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha wananchi wa Kata za Buza, Vituka, Makangarawe na Sandali katika Manispaa ya Temeke wanapata huduma ya maji, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Usambazaji Maji wa JET-Buza ambao hadi kufikia mwezi Agosti, 2023, utekelezaji umeweza kufikia asilimia 30 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024. Mradi huo utanufaisha wananchi zaidi ya 173,810 wa Kata hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika kuboresha huduma ya maji katika Mkoa wa Dar es Salaam, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 itaanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji utakaonufaisha Jimbo la uchaguzi la Temeke, Kata za Buza, Vituka, Makangarawe na Sandali pamoja na Majimbo mengine matano ya uchaguzi ya Kibamba, Ubungo, Kinyerezi, Ukonga na Ilala. Kazi zilizopangwa kufanyika ni pamoja na ujenzi wa tenki la lita milioni tisa eneo la Bangulo na ulazi wa mtandao wa mabomba wa umbali wa kilometa 124. Mradi huo unatarijiwa kukamilika ifikapo Desemba, 2024.