Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka huduma ya maji ya DAWASA katika Kata za Buza, Vituka, Makangarawe na Sandali - Temeke?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini je, sasa Serikali haioni ipo haja ya visima vile ambavyo vilichukuliwa na DAWASA ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam viweze kurudishwa mikononi mwa wananchi, kwa sababu tangu vilipochukuliwa mpaka sasa hakuna marekebsho yoyote na ndiyo maana tunakosa maji mahali pengine kwa sababu visima vilikuwa ni vingi lakini DAWASA hawavifanyii kazi. Hivyo virudishwe kwa wananchi ili maji yaendelee kupatikana kulingana na hizi asilimia 30 mlizosema mpaka sasa yanapatikana?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili je, lini Serikali sasa mtarekebisha au mtaweka mabomba, kwani yaliyopo ni chakavu a ya zamani sana ambapo sasa hivi yanatitirisha maji tu na ni upotevu tu wa maji kwa Serikali lakini sasa tuombe muweze kuyarekebisha na wananchi tuendelee kupata maji safi katika mabomba ya majumbani? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawilii ya nyongeza ya Mheshimiwa Dorothy Kilave, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, visima vilivyochukuliwa kurudishwa kwa wananachi, visima hivi vilichukuliwa kwa sababu za kiufundi. Sasa hivi namna ambavyo kwa mfano Wizara ya Afya inaweza kumiliki hospitali zake, nasi Wizara ya Maji tunahitaji kumiliki vyanzo hivi vya maji vyote ili viwe chini ya uangalizi wa wataalam wetu. Kwa hiyo, cha kufanya hapa hatutavirudisha kwa wananchi bali tutaongeza nguvu kuhakikisha visima hivi vinakwenda kutumika na kuongeza usambazaji wa maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubadili mabomba chakavu tayari hili lipo kwenye mkakati wa mwaka huu wa fedha 2023/2024 utaona Mheshimiwa Mbunge kazi huko namna ambavyo vijana wanachakarika. Nimpongeze sana CEO wa DAWASA ameingia kwa kasi na watendaji wake wote wanafanya kazi kwa kasi. Wiki iliyopita nimefanya ziara pamoja na DAWASA maeneo haya yote ninayozungumzia Mheshimiwa Kilave, nimeweza kuyapitia.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka huduma ya maji ya DAWASA katika Kata za Buza, Vituka, Makangarawe na Sandali - Temeke?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nataka kujua wananchi wa Kata ya Kamoli hutembea muda mrefu kufata chanzo cha Kitagata ambacho hakijatengenezwa vizuri, hivyo kukanyaga maji na kuchota maji machafu. Nataka nijue mkakati uliopo kuimarisha hicho chanzo cha maji lakini yakivutwa ili kuwa karibu na makazi ya watu badada ya kutembea umbali mrefu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata hii ya Kamoli kuboresha chanzo na kuleta usambazaji. Katika mwaka huu wa fedha Mheshimiwa Mbunge kuna kazi itafanyika kuona kwamba chanzo hiki kinaendelea kuwa toshelevu kinakuwa endelevu na usambazaji wa kuwasogezea huduma wananchi ni moja ya kazi yetu mama Wizara ya Maji, tutafanya hilo Mheshimiwa Mbunge.