Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 88 2023-09-05

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-

Je, ni maprofesa wangapi wanaozalishwa kila mwaka na ni wangapi wanastaafu kwa kipindi hicho?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Profesa ni ngazi ya kitaaluma ambapo Mhadhiri au Mtumishi wa Taasisi za Elimu ya Juu hufikia baada ya matokeo ya kazi za kitaaluma ikiwemo kufanya machapisho na ufundishaji. Hivyo, kupanda cheo cha mwanataaluma kunatokana na jitihada za mhusika katika ufundishaji, kufanya tafiti na kuchapisha maandiko yake katika majarida yanayotambulika Kitaifa na Kimataifa. Hivyo, kuongezeka kwa idadi yao kunategemea zaidi jitihadi za mtu binafsi katika utekelezaji wa majukumu yake na kukubalika kwa jitihada hizo kwa wanataaluma wenziwe kwa kuzingatia miongozo waliyojiwekea. Hadi kufikia Mwaka 2022 tulikuwa na jumla ya Maprofesa 226 kati yao 163 wakiwa ni Maprofesa Washiriki (Associate Professors) na 63 ni Maprofesa Kamili (Full Professors).

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kustaafu linahusu zaidi Vyuo Vikuu vya Umma ambao umri wa kustaafu ni miaka 65. Kwa takwimu za mwaka 2022 idadi ya maprofesa kamili waliostaafu ni wanne na wanaotarajia kustaafu kwa mwaka 2023 ni watano, kwa mwaka 2024 ni Wawili, na mwaka 2025 ni sita. Maprofesa Washiriki waliostaafu kwa mwaka 2022 ni mmoja na wanaotarajiwa kustaafu kwa mwaka 2023 ni 18, mwaka 2024 ni wanne, na mwaka 2025 ni sita. Ninakushukuru.