Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 96 2023-09-06

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni asilimia ngapi ya Watanzania wameandikishwa na kupatiwa Vitambulisho vya Taifa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: =

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia Tarehe 31 Julai, 2023, jumla ya Watanzania 11,242,736 wamepewa vitambulisho, sawa na asilimia 55 ya lengo la kuwapatia wananchi 20,294,910 wanaostahili kupewa. Mpango wa Serikali ni kuwagawia vitambulisho Watanzania waliobaki ifikapo Machi, 2024, ninakushukuru.