Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA K.n.y. MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni asilimia ngapi ya Watanzania wameandikishwa na kupatiwa Vitambulisho vya Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ninaomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

a) Je, ni kwa nini Serikali inachukua muda mrefu kutoa vitambulisho kwa Watanzania, hamuoni kwamba mnawakosesha fursa mbalimbali ambapo kitambulisho ndiyo takwa la fursa hizo?

b) Je, ni lini Serikali itaoanisha data zote za msingi ili ziweze kusomeka kwenye kitambulisho hicho cha NIDA?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa maswali haya mawili ya nyongeza. Naomba kutoa majibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Matiko, amekuwa mara kadhaa akifuatilia kuona namna ambavyo Watanzania wanaweza kupata vitambulisho ili kuweza kupata huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haijachukua muda mrefu sana kutoa vitambulisho kwa watu; na kama imechukua basi tulikuwa tuna changamoto. Changamoto ya kwanza tulikuwa na upungufu wa mashine za kisasa ambazo zilikuwa zinatoa vitambulisho kwa speed kubwa. Niwaambie wananchi na Watanzania; sasa tumeshapata mashine bora za kisasa na tunakwenda kuhakikisha Watanzania wote wanapata vitambulisho ili waweze kupata huduma, kwa sababu tunatambua sasa hivi kila kitu ni kitambulisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto nyingine. ninawomba Watanzania wote, wakamilishe taratibu ili tuweze kupata vitambulisho. Kuna watu wanashindwa kutoa baadhi ya particulars muhimu za kutengenezewa vitambulisho. Inakuwa ngumu kwetu kuweza kuwakamilishia.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kwamba tunavyo vitambulisho vingi. Tuone namna ya kuviunganisha vitambulisho hivyo ili kiwe kimoja. Maana yake hicho hicho kiwe na uwezo wa kutumika benki, kwenye passport unaweza ukawa unakitumia kama NIDA au kitambulisho kingine. Tuko mbioni kuona namna ambavyo Serikali itapunguza changamoto hiyo, ninakushukuru.