Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 97 2023-09-06

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, lini mabwawa ya mifugo yatachimbwa Kata za Lagama, Masanga Mwamalasa, Ngofila, Bunambiyu, Mwasubi na Somagedi – Kishapu?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo katika maeneo mbalimbali hapa nchini ikiwemo katika Jimbo la Kishapu. Kazi ya ujenzi wa mabwawa hufanyika kwa hatua kuu tatu ambazo ni; kutafuta chanzo cha maji (water source), kufanya usanifu na kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa kutambua changamoto ya upatikanaji wa maji katika jimbo la Kishapu hususani katika kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge, naomba kutoa wito kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwa kushirikiana na wataalam wa Wakala ya Huduma na Usafi wa Maji Vijijini (RUWASA), kuanza kazi ya kutafuta chanzo cha maji katika maeneo husika, kuandaa michoro (design) na mchanganuo wa gharama (BOQ) ili kuweza kupewa kipaumbele kwenye mpango na bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kutoa wito kwa wafugaji na wadau wengine, kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya maji ya mifugo ili kusaidia kupunguza changamoto ya maji kwa ajili ya mifugo hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.