Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 100 2023-09-06

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala hadi Masasi utaanza?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile ni mara yangu ya kwanza toka Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameniteua kumsaidia katika jukumu la Waziri wa Ujenzi, kwa kibali chako naomba kwanza nianze kwa kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini. Namwahidi Mheshimiwa Rais sitomwangusha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii pia kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, Mhandisi Godfrey Kasekenya, kwa kuendelea kuaminiwa na Mheshimiwa Rais. Namwahidi Mheshimiwa Rais, tutafanya kazi kwa bidii tutapambana na kudhibiti rushwa hasa kwenye maeneo ya mikataba, manunuzi na usimamizi wa miradi ili dhamira ya Mheshimiwa Rais na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi uende vyema kama tulivyowaahidi Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmed Katani, Mbunge wa Tandahimba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala – Masasi yenye urefu wa kilometa 210 unatekelezwa kwa awamu ambapo ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya Mtwara – Mnivata yenye urefu wa kilomita 50 umekamilika kwa kutumia fedha za ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sehemu ya Mnivata – Newala - Masasi yenye urefu wa kilomita 160, mikataba miwili ya ujenzi chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imesainiwa tarehe 21 Juni, 2023, kwa sehemu za Mnivata – Mitesa yenye urefu wa kilomita 100 na Mitesa – Masasi yenye urefu wa kilomita 60 pamoja na ujenzi wa Daraja la Mwiti. Kwa sasa Makandarasi wa sehemu zote mbili wapo katika hatua za maandalizi ya kuanza ujenzi, ahsante sana.