Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza:- Je, lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala hadi Masasi utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imefanya uchambuzi yakinifu wa Barabara kutoka Mtama – Mkwiti - Ng’unja – Litehu mpaka Tandahimba miaka mitatu nyuma. Je, lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa barabara hii ina kipande korofi cha kutoka Ng’unja kuja Mkwiti. Je, Serikali iko tayari kutenga fedha ya dharura kwa ajili ya kuweka lami kipande kile?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Katani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye upande wa swali la kwanza, ujenzi utaanza lini. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Katani kwa namna ambavyo amefuatilia mpaka Serikali tukafikia hatua ya kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Mara fedha zitakapopatikana ujenzi wa barabara hii utaanza mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu kipande korofi toka Ng’unja kwenda Mkwiti, Mheshimiwa Mbunge ameomba fedha za dharura. Natumia nafasi hii kuwaelekeza Mameneja wa TANROADS Mikoa yote kuangalia maeneo kama haya, maeneo korofi na kuyabainisha na kufanya assessment na kuleta Wizarani ili tunapokuwa tunaandaa bajeti, maeneo haya kama aliyoyasema Mheshimiwa Katani tuweze kuyaweka kwenye kipaumbele. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza:- Je, lini ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala hadi Masasi utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mrushaka kwenda mpaka Mrongo ilikuwa isainiwe tarehe 24 Agosti, lakini haikusainiwa ni lini barabara hii itasainiwa kwa umuhimu wa wananchi wa Kyerwa na Karagwe? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, wajina wangu na jirani yangu kule Jimbo la Kyerwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu mara tu Mheshimiwa Rais, aliponiamini na kunileta Wizara hii, moja ya simu niliyoipata ilikuwa ya Mheshimiwa Innocent Bilakwate akiulizia barabara hii. Nikamwahidi kwamba naomba awe na subira, niape kwanza halafu nitakapokuja ofisini basi tuangalie cha kufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kukaa na Mheshimiwa Mbunge na kwa vile hii barabara inapita Jimbo la Karagwe, nimegundua kwa Waheshimiwa Wabunge wengi ipo mikataba ambayo inasubiria kusainiwa kama hii ya Mheshimiwa Bilakwate, kwa hiyo, hatutowachelewesha. Nimeshamwelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi kufanya haraka iwezekanavyo ili mikataba hii isainiwe, Wakandarasi waanze hatua za ujenzi wa barabara hizi, ahsante sana. (Makofi)