Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 102 2023-09-06

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nangomba hadi Nanyumbu kwa kiwango cha lami?

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Yahya Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) tayari imekamilisha kazi za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Nangomba – Nanyumbu yenye urefu wa kilometa 28.32 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante sana. (Makofi)