Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nangomba hadi Nanyumbu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niipongeze Serikali kwa jitihada inazofanya katika kuhakikisha miundombinu yetu inakuwa mizuri, lakini naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika barabara hii ninayoitaja ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tatu, Mzee wetu Hayati Benjamin William Mkapa, ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hili ambalo mimi nauliza. Sasa ni miaka 25, Serikali bado inatafuta pesa kwa ajili ya kukamilisha barabara hii. Je, Waziri atakuwa tayari katika mwaka huu kuingiza mpango ili mwaka ujao wa fedha, barabara hii ianze kutengenezwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Jimbo la Nanyumbu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, ningependa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge kwamba ahadi za viongozi wetu Waheshimiwa Marais Wastaafu na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, zinatekelezwa, inaweza ikachelewa lakini haimaanishi kwamba hazitatekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameongea kwa hisia kali hapa kwamba ni miaka 25 toka mpendwa wetu Hayati Rais Mstaafu Benjamin Mkapa ameahidi hatujaanza utekelezaji wa barabara hii. Nimhakikishie kwamba, nitafuatilia barabara hii ili hata kama tunaanza kidogo, ilimradi tuanze kutekeleza ahadi za Viongozi wetu, ahsante sana. (Makofi)